Posts

Showing posts from February, 2019

mashine 138 za kamari zawachina mbaloni

Image
Wachina hao wamekamatwa mkoani Dodoma walikokuwa wakisambaza mashine hizo bila ya kibali na pia Wanatuhumiwa kutoa rushwa ya shilingi milioni 1 kwa Askari wa Jeshi la Polisi ambao pia.inaripotiwa kukamatwa chanzo jamii forum

Dereva wa kitanzania asababisha ajari nchini Congo

Image
Ramani ya Lubumbashi, DRC Watu 18 wamepoteza maisha na wengine 12 kujeruhiwa katika ajali ya barabarani iliyotokea Jumatano jioni katika kijiji cha Kabwe, mjini Lubumbashi, nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC). Taarifa zinasema dereva wa lori hilo ambaye ni raia wa Tanzania amekamatwa na kuwekwa rumande ikidaiwa kwamba alikuwa amelewa wakati akiendesha lori hilo. Ajali hiyo ilikuwa baina ya lori iliyokuwa imebeba tindikali ilioligonga basi la abiriya liliokuwa limesimama kituoni, wamesema viongozi wa Wizara ya Afya nchini humo. Lakini shirika moja la kiraia lililoongea na mwandishi wa Sauti ya Amerika mjini Lubumbashi, nakumfahamisha kuwa watu 30 ndio waliopoteza maisha katika ajali hiyo. Ripoti zaidi zinasema lori hilo ambalo lilikuwa linasafirisha tindikali kwenda kwenye mgodi unaozalisha madini aina ya Cobalt kwenye mji wa Kolowezi, lilikuwa linatembea kwa mwendo wa kasi. chanzo https://www.business-standard.com/ picha na  Independent Media

Miili 24 kuopolewa ikiwa imekufa

Image
Waokoaji nchini Zimbabwe wameiopoa miili 24 ya watu waliokufa kwenye migodi miwili ya dhahabu iliyokumbwa na mafuriko mnamo siku ya Jumamosi. Watu wengine wanane wameokolewa. Kwa mujibu wa televisheni ya taifa, kuna hofu kwamba wachimbaji kadhaa walio nchini humo kinyume cha sheria bado wamekwama ndani ya migodi hiyo. Shughuli za uokozi bado zinaendelea katika migodi hiyo ambayo ilikuwa haitumiwi karibu na mji wa Kadona ulipo kilomita 145 kusini magharibi mwa mji mkuu Harare. Mnamo siku ya Ijumaa serikali ilitangaza juu ya kukwama kwenye migodi hiyo miwili wachimbaji wapatao 60 hadi 70. chanzo www.aljazeera.com

KARIBU UPATE SOKO NA UNUNUE BIDHAA BORA KWA UHAKIKA

Image
Karibu kwenye blog yetu maana TUMEKUSIKIA Njoo ununue na uuze chochote kupitia blog inayokuunganisha na wateja popote ulimwenguni UZA NA NUNUA CHOCHOTE

Papa amvua Kardinali Theodore McCarrick madaraka kwa kubaka mtoto miaka 50 iliyopita

Image
Papa Francis amemvua madaraka Kardinali wa zamani, ikiwa ni tukio la kwanza kwa Kanisa Katoliki kuchukua hatua baada ya Mmarekani huyo, Theodore McCarrick kutuhumiwa kumbaka mtoto miaka 50 iliyopita, taarifa ya Vatican imesema jana. McCarrick, 88, ambaye alijitoa kutoka Taasisi ya Makardinali ya Vatican mwezi Julai, ni Kardinali wa kwanza duniani kutengwa kutokana na tuhuma za ngono. Mahakama ya Vatican ilimkuta na hatia ya kosa la kumbaka mtoto mwenye umri chini ya miaka 20, uamuzi uliothibitishwa na Papa mwezi huu, na hivyo hauwezi kupingwa zaidi, kwa mujibu wa taarifa hiyo. Ilisema McCarrick alipatikana na hatia ya “kuzini kinyume na amri ya sita kwa kufanya uzinzi na mtoto pamoja na watu wazima, na tatizo kubwa zaidi ni kutumia vibaya madaraka”. Taarifa hiyo inahitimisha kuanguka kwa aina yake kwa kardinali huyo aliyekuwa na ushawishi mkubwa na kumekuja kabla ya mkutano wa Vatican utakaofanyika Februari 21-24, ukihusisha maaskofu kutoka kila kona ya dunia kujadili namna ya kulinda ...