Umekua ukiwaza juu ya mafanikio yako? jifunze jambo hapa
Mafanikio ni nini?
Nimekaa nakuwaza kwanini kila mmoja
anataka kuafanikiwa? haijalishi watu wote hutamani kufanikiwa lakini
waliofanikiwa bado si kila anaetaka kufanikiwa yaani leo huyu kafanikiwa huyu
kaachwa na yawezekana wote walikua wanapambana kwa pamoja au yawezekana
walifanya aina moja ya shughuri lakini katika suala la kufanikiwa huyu yuko juu
huyu bado analia.
kuna vitu kadha nataka nikushuhudie
utaviangalia kwa mda wako utagundua jamboleo naanza na jambo moja
MARAFIKI
Kati
ya vitu ambavyo hujui vimekuweka hapo ulipo na kukufanya uwaze au usiwaze zaidi ufanikiwe au uzidi kua wakulialia ni aina
ya marafiki
unaowashikilia na namna unavyoishi nao. Unaweza kusema huyu anajaribu kusema nini hebu endelea kusoma
nikupe ushuhda utakusaidia kufungua akili yako ujue kua ninachokwambia kina
ukweli ndani yake.
katika
ulimwengu wa marafiki kuna aina tofauti tofauti zaidi ya kumi, leo nitakupa aina mbili tuu za marafiki siku nyingine
nitakupa aina nyingine. Marafiki wa:
1.
kukatisha tamaa uwazapo jambo jipya
hawa ukija na jambo kama hajawahi
kuliona, atakutisha tuu akikwambia rafiki yangu hapo usijaribu hufiki mbali na
kuleta mifano ya watu walio jaribu kufanya kama wewe lakini walifeli,
Hasara yao
a.
hawawezi kuja na mfano
wa mtu aliefanikiwa kwa kufanya kama wewe.
b.
Hawawezi kukuletea
mawazo ya ni njia zipi zilisababisha wale waliofeli wakashindwa.
c.
Hawezi kukupa njia
mbadala ya kufanya kupitia hilo wazo.
d.
Mara nyingi hawana
jambo jipya la kufanya.
Faida yao: hukushitua
kujua hatari zinazoweza kutokea baada ya kufanya ulichokua umekusudia hii
ukusaidia usiende kichwa kichwa.
Ushauri wangu kwako:
usikae mbali na marafiki wa aina hii tena jitahidi kuwashirikisha kila mara
uwazapo jambo jipya la kufanya.
2.
Wenye kukutia moyo
lakini hawawezi kuthubutu
Aina ya pili ya marafiki ni wale
wanao kutia moyo kila uwaambiapo unataka kufanya jambo fulani linaloweza
kukutoa ulipo. Hawa huona jambo unalowashirikisha katika hali ya mafanikio
lakini ni hawawezi kukuza (kumodify) wao ukubali na kusema iko sawa lakini
hawawezi kuona kinachoweza kutokea baada ya kufanya huona tu mafanikio na mara
nyingi hua na mifano ya watu waliofanikiwa kwa mpango huo uliouwaza.
Hasara yao
Hasara yao kubwa ni
a.
hawawezi kukupa
changamoto unazoweza kukutana nazo ukishaanza kazi hiyo wakiogopa wakisema
utavunjika moyo.
b.
Mara nyigi
ukiwashirikisha wanapiga chenga kuwa washirika wakiogopa wasipatwe na hasara (husubiri
upige hatua kwanza huku wakiwa nyuma wanakutia moyo kwa maneno yao mazuri)
c.
Ni waoga wa kutoa
maoni ya kukujenga zaidi
Faida yao:
Mara zote ni watu wanaotia moyo pale unapoonekana kukwama.
Ushauri wangu: usikae
mbali na rafiki wa aina hii maana watakufanya usonge mbele usije kukata nia
hata siku moja.
Marafiki
hawa wawili ukiwakosa huwezi kutoka ulipo na kati ya makosa makubwa
tunayoyafanya ni kuwakwepa marafiki wa kundi la kwanza na kuambatana sana na
marafiki wa la pili. Nataka nikwambie hivi kukimbia changamoto sio kuepuka
changamoto bali ni kwamba umerudi nyuma tuu huwezi kusonga mbele.
Fanya
hivi: kaa na marafiki wako hao kwa uwiano mzuri
ukiunganisha na lengo uliloleta, orodhesha mambo yote waliyo kushauri wote
wawili mmoja kwa changamoto mwingine kwa mifano ya waliofanikiwa, kaa mwenyewe
chunguza kundi waliofeli upate sababu ziorodheshe, angalia waliofanikiwa
kwanini halafu orodhesha.
Ukishajumlisha
yote jiulize unataka kufanya kwa mfumo gani mpya ambao haukuonekana pale? Halafu
je umejipanagaje mpaka sasa? Kusanya nyenzo zako anza kazi nakushuhudia hivi
utawapenda marafiki zako wote wa makundi mawili wakati unasonga mbele.
Katika mada nyingine nitakuonesha
namna ya kukaa nao wakati unasonga mbele ili usije kuporomoka na kujutia.
JAMBO
KUBWA USILOLIFAHAMU KATIKA MAFANIKIO
Kila
hatua unayoipiga kwenda mbele kutoka kwenye shimo inahitaji uwe umeshiba una
nguvu za kukutosha, hatua mia mbili kurudi ndani ya shimo hazihikuhitaji uwe
umekunywa hata maji ni rahisi sana. Yaani ni rahisi kuugua kuliko kupona.
kumbuka:
SONGA MBELE UKIZIANGALIA NA KUZILINDA HATUA ZAKO.
kumbuka:
- mafaniko hayaji kwa siku moja.
- mafanikio huwaijia wasiokata tamaa dhidi ya changamoto na kuzitatua.
- mafanikio huwahitaji waliomaanisha kuyatafuta sio waliotamani kuyatafuta.
SONGA MBELE UKIZIANGALIA NA KUZILINDA HATUA ZAKO.
Comments
Post a Comment