Siri ya mafanikio

kama unafikiri kuna pesa inayopatikana kirahisi sana umepotea

Ukikaa usikilize mawazo ya makampuni ya kubeti ambayo hutoa tumaini la kulala maskini Na kuamka tajiri ujue unapoteza mda bure.

Huwezi kuwa mtu mwenye mafanikio bila kufanya kazi hakuna kitu kulicho rahisi katika ulimwengu huu labda Mwenyezi Mungu atoe ujumbe mpya tofauti Na ule wa utakula kwa jasho

Nakwambia hivi fuatilia uone kama kuna mtu aliyepiga hatua kimaendeleo atakwambia yeye alibahatisha kupitia sportpesa, mbet, Biko au Tatu Mzuka.

Mafanikio sio kubahatisha ni mambo yafuatayo yametendeka kwa uaminifu:

1. Uchaguzi
2. Uthubutu
3. Utayari
4. Uwajibikaji
5. Umakini

Kwanza chagua kufanya kazi sio kutegeshea kupata pesa.
Ukishachagua thubutu kufanya bila woga huku

ukiwa Tiyari kwa lolote changamoto ushindi, kuanguka Na kuinuka Na kusonga mbele bila kukata tamaa

Huku ukiwajibika mda wote bila kumwachia mwingine awajibike badala yako eti unamuachia sportpesa afanye kazi wewe uamke milionea 😀😀😀😀😀 utasubiri mpaka uzeeke.

Jambo lolote ukilifanya bila umakini tegemea kufeli tuu. Sikukatishi tamaa ila hutoboi ndugu yangu mfano umefungua kibanda unaemea unaweka kibanda kinajaa unauza yanaisha unaleta unauza hujui ongezeko hujui hasara hujui mategemeo baada ya mauzo halafu unaweka mtu anauza huna list ya umeleta nini unategemea nini baada ya mauzo

Nakwambia utaemea mpaka uzeeke maana unatengeneza faida Unafanya matumizi bila kujua umeingiza shilingi ngapi hujui unakula faida yote maadamu kibanda kimejaa ujue umekosa umakini utafanya kazi miaka mingi lakini maendeleo kidogo

Chukua hatua .

Haya mambo hataki hasira mimi mwenyewe bado napambana 😂😂😂😂😂😂

Karibu WhatsApp upate mambo motomoto Na mijadala muhiku kwa kubofya kwenye neno WhatsApp hapo chini
WhatsApp

Comments

Popular posts from this blog

Rangi za plate namba na maana zake Tanzania

Ijue zaidi biashara ya juice

Namna unavyoweza kutengeneza biashara kubwa kwa kuanzia mtaji mdogo wa shilingi 10000