Augustinian hypothesis



MUHUTASARI WA NADHARIA YA AUGUSTINO MTAKATIFU (Augustinian hypothesis)
Agostino alizaliwa tarehe 13 Novemba 354 katika mji wa Thagaste mkoa wa Numidia nchini Algeria. Ni miaka michache tu baada ya ukristo kupewa uhuru wake na dola ya Kirumi mnamo mwaka 313 chini ya utawala wa mfalme Konstantino. Jina lake aliitwa  Aurelius Augustinus mara baada ya kuzaliwa. Baba yake aliitwa Patrisi anasadikika kutokua mkristo bali aliabudu miungu mingi, inasemekana amekubali na kubatizwa mwishoni mwa maisha yake. Na mama yake ni Monika, mpaka sasa anaheshimiwa kama mtakatifu alikua mkristo kweli aliyemuwezesha mwanae Konstatino kukulia maisha ya ukristo na kumlea kiimani.
Tofauti na kulelewa katika maisha mazuri ya ukristo na mama yake bado Agustino wakati wa ujana wake aliishi maisha ya anasa na uzushi, baadae alifanikiwa kupata elimu katika lugha na uwezo wa kuhubiri huko Thagaste. Aliongoka mwaka 386 na kubatizwa mwaka 387 usiku wa kuamkia pasaka na askofu Ambrosi, hapo ukiangalia alikua na miaka 32. Baada ya kubatizwa aliishi maisha ya kitawa na mnamo mwaka 391 akapewa daraja la upadre katika mji wa Hippo alioutumikia mpaka mwaka 395, na miaka miwili baadae (mwaka 397) akateuliwa kua askofu wa jimbo la Hippo. Baada yakuingia rasmi katika kazi ya Mungu alijitoa kwa kila namna kuhakikisha anafundisha, anaelekeza na kufafanua mafundisho sahihi ya ukristo ili kuwaelekeza wakristo katika kumtumikia Mungu kwa usahihi (yaani alilenga kweli haswa) kuliko vitu vingine. Aliandika maandiko mengi zaidi yenye mafundisho ya kiroho ndani yake yanayofuatwa na watu wengi mpaka sasa.
Inasaidikika kati ya mababa wa kanisa ndiye baba wa kanisa aliyeacha maandishi mengi zaidi, Maltin Luther mwenyewe amekiri kua Augustino amekua baba wake wa kiroho pamoja na Paulo. Baadhi ya maandiko yake ni
Ni miongoni mwa waandishi walioandika nadharia mbalimbali ikiwepo nadharia ya matatizo ya kisinoptiki katika agano jipya inayozihusisha injili za Mathayo, Marko na Luka, nadharia hii ndiyo tutakayoiangalia kwa undani.
Nadharia ya Augustino
Hii ni nadharia inayojaribu kutoa majibu ya injili ipi iliandikwa ya kwanza kati ya Mathayo, Marko na Luka, ambapo alisema Mwinjilist Mathayo aliandika injili yake akiwa wa kwanza baadae akafuatia Marko ambaye alitumia maandiko ya Mathayo na mafundisho ya Peter (aliyesadikika kutembea nae pamoja katika ziara mbalimbali za kueneza injili ya Kristo) kama chanzo. Pia alisema kua Mwinjilist Luka ndiye aliyeandika baadae akizitumia injili za Mathayo na Luka katika uandishi wake kama inavyoelezwa katika kitabu cha Luka 1:1-4. Tofauti ya nadharia hii na nyingine ni kwamba Augustino amejikita zaidi katika ushaidi wa kihistoria kupitia maandiko yaliyoandikwa na mababa wa kanisa mapema mwa karne ya pili ambayo bado yalikua yakishikiliwa na wakristo bila kuangalia mfumo wa kiuandishi katika injili hizo tatu.
Wafuasi wa maandiko ya nadharia ya Augustino waliona kua nadharia yake ni nyepesi na yenye mawazo yakufikirika zidi ya matatizo ya kisnoptiki. Nadharia hii ilizua maswali mengi kama vile ni kwa namna gani mila za ukristo wa kwanza zitegemewe, injili ipi iliandikwa kwanza sasa, je kuna chanzo kilichofichika nyuma?, haya na mengine yaliibuka ambayo yalichochea uandishi wa nadharia nyingine ili kuleta ukweli wa injili ipi iliandikwa kwanza, kama vile nadharia ya vyanzo viwili, uhusiano wa nadharia ya chanzo-Q, nadharia ya Farrer na nyinginezo.
Maeneo mengine makuu mawili ya ubishi kwenye jumuiya ya Augustino ni juu ya injili ya Mathayo kama mwanzo iliandikwa katika lugha ya kiebrania au iliyoandikwa kwa Kiyunani ndio ya mwanzo iliyoandikwa na mwinjilisti Mathayo. Pia kulikua na ubishi wa nani ameandika akiwa wa kwanza kati ya Marko na Luka, nadharia ya Griesbach (Griesbach hypothesis) inasadikika kubadili kidogo nadharia ya Augustino na kukubalia na kwamba Mathayo aliandika akifuatiwa na Marko pia Luka ila haiongelei kama injili ya Mathayo ilikua ya kiebrania kwanza au kiyunani hivyo ikahesabia kama marekebisho ya nadharia ya Augustino.
Baadhi ya mababa wa kanisa walioandika juu ya mpangilio wa injili kama Irenaeus, Origen, Eusebius na wengine walikuabaliana na mawazo ya Augustino kua Mathayo aliandika wa kwanza katika lugha ya kiebrania akifuatiwa na Marko pia Luka. Tuangalie ushaidi wao kwa ufupi;
Papias: Kulingana na maelezo ya Iranaeus, Papious ni miongoni mwa mashuhuda wa John pamoja na Polycarp zamani hizo nae pia katika kitabu chake alisema kua Mwinjilisti Mathayo aliandika injili akiwa wa kwanza. Aliandika kwamba “Mathayo alikusanya maoni yake katika lugha ya kiebrania na kila mmoja akatafsiri katika lugha yake awezavyo”.
Clement:  Eusebius pia alinuukuu jumbe muhimu kutoka kwa Clement wa Alexandria:  alikua akisema kua Injili za kwanza ni Mathayo na Luka ila injili ya Marko ilitokea baada ya Marko kua na Peter katika kueneza injili huko Rumi, wakati huo aliweza kusikiliza yote yaliyosemwa na Petero kama injili ya Yesu na kuaandika ili yatumike kwa wote watakaohitaji kupata mafundisho hayo, Petero alipata taarifa hizo na hakupinga au kutia mkazo sana.
Irenaeus:  Irenaeus aliyekua akijua juu ya kazi ya Papias na akimjua Polycarp na inasemekana alimjua pia mtume Yohana aliandika akisema: “ Sasa Mathayo alichapisha kitabu chake cha inijili kwa lugha ya kiebrania mwenyewe, wakati huo Petero na Paulo walikua wakihubiri injili Rumi na kuanzisha kanisa. Yeye alitofautiana na wenzake kwa kusema kua injili ya Marko iliandikwa baada ya kifo cha mtume Petro na wakati Papias na Clement walisema Petro alikuwepo nakuiona kazi ya Marko. Lakini hii haikua hoja ya kukataa nadharia ya Augustino maana yeye hakuongelea kuwepo au kutokuwepo kwa Petro katika kipindi cha uandishi wa injili ya Marko.
Tunaweza kuona na kutambua mchango mkubwa wa nadharia ya Augustino mtakatifu ilivyoweza kufungua milango ya mahojiano zaidi ili kujua ni injili ipi iliandikwa kwanza katika mpangilio wa injili tatu za kisnoptiki.

Comments

Popular posts from this blog

Rangi za plate namba na maana zake Tanzania

Ijue zaidi biashara ya juice

Namna unavyoweza kutengeneza biashara kubwa kwa kuanzia mtaji mdogo wa shilingi 10000