Matendo ya mpasayo kutenda au kuacha kwa muislamu (akhlaq)


Matendo ya mpasayo kutenda au kuacha muislamu [Moral obligations (akhlaq)]
Hizi ni sharia ambazo kila muislam azitimize, na sharia hizi zinaelekea kufanana na za kitabu cha agano la kale. Baadhi ya sharia kama kutokuua, kutokuiba, kutokushuhudia uongo zote pia zinapatikana katika quran na kitabu cha agano la kale, mfano wa sharia zile zinazo patikana kwenye sura 17:31-39 zimebeba maneno mengi yanayopatika kweneye agano la kale.
Ili tendo lolote kuhukumiwa ni zuri au baya linategemea taratibu zilizowekwa ambazo zimegawanyika katika makundi mawili; zile ambazo ni nzuri yaani zinazoonesha unyeneyekevu wa mwanadamu kwa Mungu nazo huitwa mar’ufat na zile mbaya zinazoonesha uasi wa mwanadamu kwa Mungu hizi huitwa munkarat.
Sehemu hiyo ya kwanza bado huigawa katika sehemu nyingine tatu:
1.      Fardh: haya ni yale matendo ya lazima kwa kila muislamu kama kujitimiza nguzo tano za uislam hapa mtu ataadhibiwa kwa kutokuzifuata na kufuata mafundisho ya uislamu. Ndani ya kundi hili pia kuna zile zinaitwa wajib ambayo ni matendo anayotenda muislam lakini haadhibiwi kwa kutokuyatenda pia kama kusaidia yatima mwishoni mwa kipindi cha mfungo au kabla ya sala ya idd.
2.      Marufat: haya ni matendo ambayo yanasisitizwa kufanywa na hujulikana Zaidi kama mandub yanasemekana kutokana Zaidi na uongezaji au upunguzaji wa mambo ya kitamaduni ya zamani pamoja na misemo ya Muhammad. Mambo haya yanachukuliwa kua mema kuyafanya kuliko kuyaacha mojawapo ni kuuona mwezi uliochomoza.
3.      Mubah,jai’z au halal: haya ni yale matendo ambayo muislamu huruhusiwa kufanya ila ni ya hiari hutaadhibwa usipoyafanya.
Munkarat pia imegawanyika katika sehemu kuu mbili
a.       Haram: ni matendo ambayo kila muislamu hapaswi kuyafanya na haya husababisha adhabu kutoka kwa Mungu, haya hujumuisha dhambi kubwa kama kuvunja moja wapo ya sharia, au kuvunja ahadi, kujiua, kulala na mwanamke aliye kwenye siku zake.
b.      Makruh: haya ni yale matendo ambayo adhabu yake sio kubwa sana lakini kwa muislamu mwenye iman anaejua anachokifanya hapaswi kuyafanya kama kutamka sala ukiwa na njaa, kuvunja mojawapo ya matendo madogo kwenye jamii, Zaidi ya haram na makruh kuna matendo ya kijumla ambayo muislam hapaswi kufanya kama kuvunja mojawapo ya majukumu ambayo Muhammad alifanya. Maelezo haya yamehakikiwa vyema kutoka vyanzo zaidi ya kimoja kama inavyoonekana hapo chini. kama una elimu yoyote juu ya kilichoandikwa usiache ku comment hapo chini. pia follow kupata taarifa nyingine mpya.

VITABU NA KURASA ZA KUREJEA

Norlen, G. (2001). Islam and its World. Usa River: Makumira Publications.

Comments

Popular posts from this blog

Rangi za plate namba na maana zake Tanzania

Ijue zaidi biashara ya juice

Namna unavyoweza kutengeneza biashara kubwa kwa kuanzia mtaji mdogo wa shilingi 10000