NAWEZAJE KUFIKIA KIWANGO KIKUBWA CHA MAFANIKIO?
Tamaa Haya sasa umepata wazo ukapambana na woga ukashinda na kufanikiwa kupata maamuzi ya kuanza kitu kingine kinachoweza kuleta shida hapa ni tamaa. Tamaa huja hasa katika upande wa mafanikio tena sio tamaa tu maana asiyetamani sidhani kama anaweza kufanya jambo kwakuwa mambo mengi hutokea si tu kwa sababu ya ulivipenda mwanzo mara nyingine ulitamani baadhi ya vitu kwake na kujikuta umeanza kuviingiza kwenye akili na kujikuta unapenda sana hicho kitu na kuanza kuhitaji kukitekeleza. Ila sasa kinacholeta shida ni kule kutamani kubaya (tamaa mbaya) ambako huja kwa mtu na kutamani kila kitu kiwezekane haraka haraka, yaani mtu anahitaji leo aanze leo hii aone matunda yake. Lakini mda mwingine mtu huipoteza fursa Fulani kwakupiga mahessabu ya mafanikio tuu na kuona anaweza kupata kiasi kidogo sana cha faida na kuamua kukimbia. Je umewahi kujiuliza ni kitu gani kimefanya usiwe mbunifu na kuleta mabadiliko makubwa kwenye jambo unalolifanya? TAMAA, tamaa amekuwa adui mkubwa sana kusababis...