Posts

Showing posts from August, 2019

NAWEZAJE KUFIKIA KIWANGO KIKUBWA CHA MAFANIKIO

1. Watu Kuna watu wa aina mbili kuu utakaokutana nao wakati unajaribu kuwashirikisha katika kitu unachowaza. Watu wanaokutia moyo Hawa ni watu wazuri sana katika hatua yako ya kwanza unapaswa kukaa nao kwa karibu sana maana hukupa matumaini ya namna unavyoweza kufanikiwa kutoka katika mradi wako au biashara yako maana wakianza kukupigia faida inayotokana na biashara hiyo weeee!, watakupampu utatamani kuanza mda huo huo. Ila usiwe mtu wa haraka hapa maana bado kuna kikundi kingine muhimu hujakipata ambacho ni kikundi cha watu wa aina ya pili. Uwapo na aina hii ya watu hakikisha unajipatia taarifa zote za maongezi yao kwa kuzingatia yafuatayo: Wanonaje kama ukianzisha biashara hiyounaweza kupata faida kiasi gani? Ni vitu gani hasa ukiviongeza katika biashara hiyo vinaweza kuleta faida sana katika biashara yako Ni akina nani wamewahi kufanya biashara kama hiyo wamefanikiwa sana ni kitu gani kiliwasaidia, kwakua hawa ni watia moyo wanakuwa na orodha kibao ya watu waliotoboa kutoka k...

NAWEZAJE KUFIKIA KIWANGO KIKUBWA CHA MAFANIKIO?

Mambo ya msingi ambayo waliofanikiwa huwafanya wazidi kufanikiwa. Je mambo gani watu waliofaniukiwa na kuwafanya wafanikiwe? Na mambo gani huwa tofauti na wale ambao bado hawajafanikiwa? Ndoto Watu waliofanikiwa kwanza huwa na ndoto kubwa yaani huwaza mbali (hulenga mbali). Mtu mweny endoto kubwa siku zote hupambana kuzifikia ndoto zake ndio maana Yusuph alikuwa na ndoto ya kusimamisha mganda wake kati kati ya miganda ya ndugu zake na miganda ya ndugu zake kuinamia mganda wake. Mwanzo 37:7 hivyo ndivyo watu waliofanikiwa huota na kuamini ndoto zao huamini kusimama katikati ya walioshindwa na wao kuibuka washindi katika mambo yao. Ukiwaza juu ya mafanikio siku zote utafanikiwa tuu ukiwaza juu ya kushindwa hata usijisumbue wewe umeshindwa tuu. Hukaza mwendo siku zote. Zaidi ya ndoto kitu kingine cha tofauti kwa watu waliofanikiwa ni kukaza mwendo siku zote. Hawa ni watu ambao hawakai wakasubiri miujiza ijitokeze bali husimama imara na kusonga mbele ili kusababisha ndoto zao kutimia...

NAWEZAJE KUFIKIA KIWANGO KIKUBWA CHA MAFANIKIO?

Tamaa Haya sasa umepata wazo ukapambana na woga ukashinda na kufanikiwa kupata maamuzi ya kuanza kitu kingine kinachoweza kuleta shida hapa ni tamaa. Tamaa huja hasa katika upande wa mafanikio tena sio tamaa tu maana asiyetamani sidhani kama anaweza kufanya jambo kwakuwa mambo mengi hutokea si tu kwa sababu ya ulivipenda mwanzo mara nyingine ulitamani baadhi ya vitu kwake na kujikuta umeanza kuviingiza kwenye akili na kujikuta unapenda sana hicho kitu na kuanza kuhitaji kukitekeleza. Ila sasa kinacholeta shida ni kule kutamani kubaya (tamaa mbaya) ambako huja kwa mtu na kutamani kila kitu kiwezekane haraka haraka, yaani mtu anahitaji leo aanze leo hii aone matunda yake. Lakini mda mwingine mtu huipoteza fursa Fulani kwakupiga mahessabu ya mafanikio tuu na kuona anaweza kupata kiasi kidogo sana cha faida na kuamua kukimbia. Je umewahi kujiuliza ni kitu gani kimefanya usiwe mbunifu na kuleta mabadiliko makubwa kwenye jambo unalolifanya? TAMAA, tamaa amekuwa adui mkubwa sana kusababis...

NAWEZAJE KUFIKIA KIWANGO KIKUBWA CHA MAFANIKIO?

3. Maamuzi Katika kipengele kilichopita tumeona woga unavyokwamisha mtu kupiga hatua kuelekea mafanikio aliyoyakusudi, sasa hapa tutazidi kuona jinsi uamuzi wako ndio suluhisho kubwa la maisha yako. Mafanikio yote hutegemea maamuzi yako kufanikiwa au kutofanikiwa hutegemea uamuzi wako mwenyewe, maamuzi huweka malengo, malengo hutoa mwelekeo na mwelekeo huchochea kujituma na kujituma huchomoza mafanikio halisi. Lakini katika kuamua hapo ndipo watu wengi hujikuta wakifeli na kuaanza kumtafta mchawi wa maendeleo yao pasipo kujua kua maamuzi yao ndio yamewafelisha. Mtu mmoja huamua kufanya kazi kwa bidii, mtu mwingine huamua kuiba, mtu mwingine huamua kwenda kwa waganga ili apate pesa akiwa amekaa, hawa wote mafanikio yao yanakuja au yanaharibika kutokana na maamuzi yao. Hivyo suala la maamuzi ndio muhimili mkubwa wa mafanikio uliyonayo au kushindwa kwako kufikia maono uliyonayo. Kwakua tulishajua kuwa kila mmoja ana uwezo wa kuanzisha wazo na kufikia mafanikio, sasa tuangalie uamuzi na...

CHA KUFANYA ILI KUWA NA MAFANIKIO MAKUBWA KIFEDHA

2. WOGA Haya sasa baada ya kupata wazo la kufanya. Watu wengi nimegundua baada ya kupata wazo la kibiashara hakuna hata mmoja anayekua mzembe kufanya utafiti, hili ni jambo muhimu sana katika aina yeyote ile ya biashara au utekelezaji wowote. Jambo ambalo linaloleta shida katika utafiti unaofanywa na mwekezaji ni asilimia kubwa ya wawekezaji hutegemea kupata taarifa nzuri zinazoongelea kitu wanachohitaji kuwekeza: Kwanza kuona orodha za watu waliowekeza katika fursa hiyo na kufanikiwa. Pili kukutana na orodha ya faida zinazotokana na uwekezaji huo tuu na si tofauti, rejea kwenye mfano wa uwekezaji wa kuku hapo juu. Tatu kuona mchanganuo wa mapato makubwa yanayoweza kupatikana kwa mda mfupi endapo utawekeza katika fursa hiyo. Lakini leo nataka nikwambie kitu usichokipenda kukisikia hakuna biashara yeyote inayoweza kukufanya uwe tajiri inaweza kukupa majibu ya aina hiyo. Ukiona hivyo ujue kuwa unafanywa tajiri kimawazo na unaishia kuwazia kuwa tajiri tuu miaka yote. Watu wote walio...

NAWEZAJE KUFIKIA KIWANGO KIKUBWA CHA MAFANIKIO?

NAWEZAJE KUFIKIA KIWANGO KIKUBWA CHA MAFANIKIO? Katika tafiti na uzoefu nilioweza kupata nimegundua kuwa kila mmoja anahangaika sana kuhakikisha anafanikiwa kimaisha, labda akiwaza kuwa tajili kama Fulani au akihitaji kufikia ndoto Fulani katika maisha yake. Lakini mambo siku zote yanakuwa hivi asilimia ndogo huweza kufikia ndoto zao na asilimia kubwa uendelea kuota pasipo kuamka usingizini, na asilimia kubwa kati ya wale waliofanikiwa kufikia ndoto zao au walio karibu kufikia ndoto zao hudumu kwa mda kisha huyumba au hufirisika. Hapa nitaweka baadhi ya mambo ambayo usipoyaangalia kwa umakini yanaweza yakakufanya uendelee kuota tuu ndo pasipo kufikia hatima ya ndoto yako au kuisahau ndoto yako: Wazo Woga Maamuzi ya wakati Tamaa 1. WAZO Mara nying watu hutafuta wafanye nini yaani ni kitu gani wawekeze kwacho. Na hili limekuwa tatizo linalosumbua watu wengi sana kufikia hadi asilimia tisini. Hii imepelekea baadhi ya watu kuweka dau kubwa ili kununua wazo la kibiashara kuytoka kwa...